Pastor Elisha M Mapande
26/11/2025
MUNGU ANA MPANGO NA WEWE.
Katika hali ya kawaida una weza kuona k**a Mungu ame kuacha na kuku telekeza.Hata k**a hauja tenda dhambi au kuanguka kiroho.
Mungu ana jivunia juu yako hata jinsi unavyo shinda majaribu na kupambania Imani yako.
Ayubu 4:7
[7]Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia?
Au hao waelekevu, walikatiliwa mbali wapi?
Wakati mwingine unapo pita kwenye changamoto fulani.Adui ana jitahidi kukufanya uone ubaya zaidi ya matendo makuu ya Mungu aliyo wahi kukutendea usikate tamaa.
Changamoto na mapito k**a haya ambayo tuna yaona kwenye kitabu cha ayubu ni Mungu anajivunia mtoto wake alivyo mwaminifu kwake hata kwenye tabu.
Yakobo 1:12
[12]Heri mtu astahimiliye majaribu; kwa sababu akiisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima, Bwana aliyowaahidia wampendao.
Nipo hapa kuku tangazia kwamba Mungu anakupenda na ile Kazi njema aliyo anzisha kwenye maisha yako ata itimiza.
Hivyo ukipita kwenye hali ya kujaribiwa uone ng'ambo ya jaribu lako ambayo ni taji ya uzima.Usione jaribu k**a teso na maumivu bali ngazi ya kupandishwa kwenda hatua nyingine.
Amini kwenye mchato wa Mungu kuifundisha mikono yako vita k**a Daudi semavyo (Zaburi 18:34
[34]Ananifundisha mikono yangu vita,
Mikono yangu ikaupinda upinde wa shaba.)
Hakika utashinda kwa msaada wa Bwana na kuingia viwango vingine.
Mwisho haya yote ni kwa wale walio mpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao.Mpokee Yesu wewe k**a bado ili uwe mrithi wa ahadi hizi amen amen.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Moshi