EBONY Digital
Frequency; Iringa 87.8, Mbeya 94.7, Dar 106.9, Njombe 88.2, Songea 102.2 MHz
31/03/2025
Kapteni Ibrahim Traoré, Rais wa Serikali ya Mpito ya Burkina Faso, ametoa msamaha kwa wanajeshi 21 waliohusika katika mapinduzi ya Septemba 2015. Amri hii, iliyosainiwa Machi 24 na kuwekwa hadharani Jumapili, inazingatia masharti ya msamaha yaliyopitishwa na bunge la mpito mnamo Desemba 2024. Wanajeshi hao, wakiwemo maafisa na maafisa wasio na kamisheni, walikuwa wamefungwa au kutiwa hatiani kwa matendo yao katika mapinduzi yaliyoshindwa ya 2015.
Sheria ya msamaha inatoa fursa kwa askari waliohusika na kesi hii, na wanaoonyesha kujitolea katika mapambano dhidi ya ugaidi, kupewa msamaha na kupandishwa cheo kazini.
29/03/2025
Uchaguzi wa chama cha soka mkoa wa Iringa umekamilika ambapo wajumbe wa mkutano mkuu wamewachagua viongozi wapya wa chaka hicho (IRFA) watakaokua madarakani kwa miaka minne ya kiutawala.
VIONGOZI WALIOCHAGULIWA NI K**A IFUATAVYO
Crypian Kuyava - Mwenyekiti
Joel Musiba - Makamu mwenyekiti
Abousufian Silia - Mjumbe wa mkutano mkuu
⛳️Wajumbe wa k**ati ya utendaji.
1. Victoria Mwenda
2. Davis Wapalila
3. Rehema Mhehe
Baada ya kupitishwa kwa makamu mwenyekiti na mkutano mkuu, kinasubiriwa kikao cha k**ati ya utendaji ambacho kitampitisha katibu atakayeteuliwa na mwenyekiti.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Address
Uhindini
Iringa
255