Southern Tanzania Elephant Program

Southern Tanzania Elephant Program

Share

Our mission is to secure a peaceful future for elephants in southern Tanzania. We support the protection efforts of rangers; work with farmers and the broader community to enhance coexistence with elephants; and advise on conservation of elephant corridors.

Photos from Southern Tanzania Elephant Program's post 16/05/2026

๐Š๐ฎ๐ญ๐จ๐ค๐š ๐Œ๐ฐ๐š๐ง๐š๐Ÿ๐ฎ๐ง๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐Œ๐š๐Ÿ๐ฎ๐ง๐ณ๐จ ๐ค๐ฐ๐š ๐•๐ข๐ญ๐ž๐ง๐๐จ ๐ก๐š๐๐ข ๐€๐Ÿ๐ข๐ฌ๐š ๐”๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข: ๐’๐š๐Ÿ๐š๐ซ๐ข ๐ฒ๐š ๐”๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข ๐ฒ๐š ๐„๐ฅ๐ข๐ณ๐š๐›๐ž๐ญ๐ก

Uhifadhi wa maeneo ya Tanzania yenye bioanuwai kubwa hauhitaji mikakati pekee, bali pia unahitaji ujasiri, kujitolea, na watu wenye dhamira ya kweli ya kulinda hifadhi zetu. Kutana na Elizabeth Masatu โ€” mmoja wa mashujaa wanaoleta mabadiliko kila siku kupitia juhudi zake za dhati katika uhifadhi.

Eliza alijiunga na shirika la STEP mwaka 2022 k**a mwanafunzi wa mafunzo kwa vitendo , na baadaye akawa Afisa Ushoroba, akisaidia urejeshwaji wa Shoroba ya Wanyamapori ya Nyerereโ€“Udzungwa katika Bonde la Kilombero. Mwaka 2024, alihamia Idara ya Uhifadhi ya STEP, ambako sasa anahudumu k**a Afisa Uhifadhi

Katika nafasi yake ya sasa, Eliza huratibu doria za pamoja na , na Askari wa Wanyamapori wa Vijiji katika maeneo matatu muhimu ya hifadhi, akisaidia kuimarisha juhudi za uhifadhi katika mandhari ya Udzungwaโ€“Kilombero. Pia anaongoza shughuli za chumba chaufuatiliaji cha STEP (control room), akisimamia mfumo wa EarthRanger kufuatilia timu za uwandani na kusaidia maamuzi ya haraka kwa ufanisi zaidi wa uhifadhi wa uwandani.

Eliza pia ni mhitimu wa programu ya Grumeti Fundโ€™s Women in the Field. Akiwa nje ya kazi ya uhifadhi, Eliza hupendelea kusafiri, kutazama filamu, na kusikiliza muziki.

K**a spishi muhimu (keystone species) katika mfumo wa ikolojia, Eliza ana mchango mkubwa katika kuimarisha na kudumisha juhudi za uhifadhi ndani ya STEP. Tunajivunia kuwa naye katika timu yetu na kushirikiana naye katika safari hii ya uhifadhi yenye msukumo mkubwa.

Photos from Southern Tanzania Elephant Program's post 09/05/2026

๐„๐ฅ๐ข๐ฆ๐ฎ ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐๐จ๐ง๐๐ž ๐ฅ๐š ๐Š๐ข๐ฅ๐จ๐ฆ๐›๐ž๐ซ๐จ

Kila mtoto mwenye ufahamu kuhusu wanyamapori leo, anachangia kujenga kesho salama zaidi kwa watu na mazingira.

Kupitia programu yetu ya uhamasishaji shuleni, wanafunzi wanaoishi karibu na maeneo ya hifadhi wanajifunza:

โœ… Hatua za usalama wanapokutana na tembo
โœ… Tahadhari wakati wa kukutana na wanyamapori
โœ… Umuhimu wa kulinda mazingira na wanyamapori katika jamii zao

Hadi sasa, tumefundisha jumla ya masomo 6 katika shule 31, ikiwemo shule 8 za sekondari. Mwaka 2025 pekee, tumefundisha:

๐Ÿ“š Wanafunzi 4,907
๐Ÿ‘ง Wasichana 2,486
๐Ÿ‘ฆ Wavulana 2,421

Vipindi hivi vya mafunzo ya elimu vimetolewa na Mwezeshaji wetu wa idara ya Kuishi kwa Ushirikiano na Wanyamapori na Maisha Endelevu (Coexistence and Livelihoods), Beatrice Lihaku. Tunamshukuru kwa dhati Beatrice kwa kazi kubwa anayofanya katika kutoa mafunzo haya kote Bonde la Kilombero.

Hii ni zaidi ya elimu โ€” ni kujenga mustakabali ambapo watu na wanyamapori wanaweza kuishi pamoja kwa usalama na uendelevu.

Photos from Southern Tanzania Elephant Program's post 02/05/2026

๐Š๐ฎ๐ฃ๐ž๐ง๐ ๐š ๐”๐จ๐ง๐ ๐จ๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐’๐ž๐ซ๐ข๐ค๐š๐ฅ๐ข ๐ณ๐š ๐Œ๐ข๐ญ๐š๐š: ๐”๐š๐ง๐ณ๐ข๐ฌ๐ก๐ฐ๐š๐ฃ๐ข ๐ฐ๐š ๐Š๐š๐ฆ๐š๐ญ๐ข ๐ฒ๐š ๐”๐ฌ๐ข๐ฆ๐š๐ฆ๐ข๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐๐š๐ฆ๐จ๐ฃ๐š ๐ฒ๐š ๐”๐ฌ๐ก๐จ๐ซ๐จ๐›๐š ๐ฐ๐š ๐๐ฒ๐ž๐ซ๐ž๐ซ๐žโ€“๐”๐๐ณ๐ฎ๐ง๐ ๐ฐ๐š

Tarehe 10 Aprili 2026, hatua muhimu ilipatikana katika Ukanda wa Wanyamapori wa Nyerereโ€“Udzungwa (NUWC) kwa kuanzishwa rasmi kwa K**ati ya Usimamizi ya Pamoja- Joint Management Committee (JMC) chini ya Kanuni za Maeneo ya Njia za Wanyamapori (ushoroba) za 2018. Hii ni hatua ya kuimarisha utawala wa ndani na uendelevu wa ushoroba wa kwanza wa wanyamapori uliotambuliwa kisheria Tanzania.

JMC inahusisha viongozi wa vijiji vya Sole, Mangโ€™ula A, na Kanyenja, pamoja na mamlaka za serikali na taasisi za uhifadhi k**a , , , , na Ofisi ya Wakili wa Halmashauri ya Ifakara ()chini ya uratibu wa STEP.

Baada ya mchakato wa uwazi wa uchaguzi na uapisho, uongozi uliundwa k**a ifuatavyo:

>Mwenyekiti โ€“ Kijiji cha Sole
>Makamu Mwenyekiti โ€“ TAWA
>Katibu โ€“ Afisa Wanyamapori wa Wilaya (MNRT)

Uanzishwaji huu unaonesha wazi kuwa jamii ziko katikati ya maamuzi ya usimamizi wa ushoroba huu, zikishirikiana na serikali na wadau wa uhifadhi.

Kwa uratibu wa kwa kushirikiana na , JMC hii ni mfano wa uongozi wa kijamii unaolenga uhifadhi shirikishi na endelevu ambapo watu na wanyamapori wanaishi kwa pamoja kwa ustawi.


**atiYaUsimamiziYaPamoja

08/03/2026

๐–๐š๐ง๐š๐ฐ๐š๐ค๐ž ๐ฐ๐š ๐’๐“๐„๐: ๐–๐š๐ค๐ข๐จ๐ง๐ ๐จ๐ณ๐š ๐”๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข ๐ค๐ฐ๐š ๐€๐ฃ๐ข๐ฅ๐ข ๐ฒ๐š ๐–๐š๐ญ๐ฎ ๐ง๐š ๐€๐ฌ๐ข๐ฅ๐ข

Katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, tunasherehekea wanawake wa STEP ambao wanachangia ujuzi wao na kujitolea kwao katika kujenga mustakabali ambapo asili na jamii vinaweza kustawi pamoja. ๐ŸŒฟ

Miongoni mwao kuna wanawake viongozi wanaoongoza idara zao kwa busara na maono, wakisaidia timu zao kukua huku wakiiimarisha taasisi kwa ujumla.

Pia tuna wanawake wanaofanya kazi uwandani, wakifanya tafiti, kusaidia kuboresha maisha ya jamii, kufanya uhifadhi katika hifadhi za asili na kushughulikia changamoto za migogoro kati ya binadamu na wanyamapori, ili kuhakikisha kuwa uhifadhi unaleta manufaa halisi kwa watu wanaoishi karibu na wanyamapori.

Wengine hufanya kazi nyuma ya pazia - ofisini, wakihakikisha fedha zinasimamiwa vizuri, ustawi wa wafanyakazi unazingatiwa, na ofisi zinabaki kuwa mahali pazuri pa kufanyia kazi. Jitihada zao zinawezesha shughuli za kila siku za STEP kuendelea vizuri.

Tunapotafakari kaulimbiu za mwaka huu โ€œ๐™ƒ๐™–๐™ ๐™ž. ๐™๐™จ๐™–๐™ฌ๐™–. ๐™ƒ๐™–๐™ฉ๐™ช๐™– ๐™ ๐™ฌ๐™– ๐™’๐™–๐™ฃ๐™–๐™ฌ๐™–๐™ ๐™š ๐™ฃ๐™– ๐™’๐™–๐™จ๐™ž๐™˜๐™๐™–๐™ฃ๐™– ๐™’๐™ค๐™ฉ๐™šโ€ na โ€œ๐™๐™ค๐™– ๐™ž๐™ก๐™ž ๐™๐™ฅ๐™–๐™ฉ๐™š,โ€tunasherehekea na kushukuru kwa kujitoa kwao, uongozi bora, huduma safi, na mchango wao mkubwa wanaoutoa wanawake wa STEP na wanawake wote katika sekta ya uhifadhi kila siku. ๐€๐ฌ๐š๐ง๐ญ๐ž๐ง๐ข ๐ฌ๐š๐ง๐š ๐ค๐ฐ๐š ๐ฆ๐œ๐ก๐š๐ง๐ ๐จ ๐ฐ๐ž๐ง๐ฎ ๐ฆ๐ณ๐ฎ๐ซ๐ข ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฃ๐š๐ฆ๐ข๐ข

Photos from Southern Tanzania Elephant Program's post 24/02/2026

๐Š๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐ž๐ณ๐š ๐‹๐ž๐จ ๐ค๐ฐ๐š ๐Š๐ข๐ณ๐š๐ณ๐ข ๐Š๐ข๐ฃ๐š๐œ๐ก๐จ ๐œ๐ก๐š ๐–๐š๐ง๐š๐ฌ๐š๐ฒ๐š๐ง๐ฌ๐ข ๐ฐ๐š ๐”๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข

Grace Mchome alijiunga na STEP mwaka 2022 k**a mwanafunzi wa Shahada ya Uzamili kupitia programu yetu ya kujenga uwezo wa utafiti na ufuatiliaji, akipata mafunzo ya ukusanyaji na uchambuzi wa data pamoja na uandishi wa kisayansi chini ya usimamizi wa Dk. Josephine Smit.

Utafiti wake katika Bonde la Kilombero ulichunguza ufanisi wa vizuizi vya kuzuia tembo k**a uzio wa mizinga ya nyuki, bati na taa za sola, akitumia mitego ya kamera na mahojiano na wakulima.

Kwa maneno ya Grace mwenyewe:โ€œ๐™†๐™ช๐™ฌ๐™–๐™จ๐™ž๐™ก๐™ž๐™–๐™ฃ๐™– ๐™ฃ๐™– ๐™Ÿ๐™–๐™ข๐™ž๐™ž ๐™ ๐™ช๐™ก๐™ž๐™Ÿ๐™š๐™ฃ๐™œ๐™– ๐™ช๐™Ÿ๐™ช๐™ฏ๐™ž ๐™ฌ๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ช ๐™ฌ๐™– ๐™ข๐™–๐™ฌ๐™–๐™จ๐™ž๐™ก๐™ž๐™–๐™ฃ๐™ค ๐™ฃ๐™– ๐™ ๐™ช๐™ฅ๐™–๐™ฃ๐™ช๐™– ๐™ช๐™š๐™ก๐™š๐™ฌ๐™– ๐™ฌ๐™–๐™ฃ๐™œ๐™ช ๐™ ๐™ช๐™๐™ช๐™จ๐™ช ๐™ช๐™๐™ž๐™›๐™–๐™™๐™๐™ž - ๐™ ๐™ฌ๐™–๐™ข๐™—๐™– ๐™จ๐™ž๐™ค ๐™ฉ๐™ช ๐™ ๐™ช๐™๐™ช๐™จ๐™ช ๐™ช๐™จ๐™ž๐™ข๐™–๐™ข๐™ž๐™ฏ๐™ž ๐™ฌ๐™– ๐™ฌ๐™–๐™ฃ๐™ฎ๐™–๐™ข๐™–๐™ฅ๐™ค๐™ง๐™ž ๐™ก๐™–๐™ ๐™ž๐™ฃ๐™ž ๐™ฅ๐™ž๐™– ๐™ ๐™ช๐™ ๐™ช๐™ฏ๐™– ๐™ช๐™จ๐™ฉ๐™–๐™ฌ๐™ž ๐™ฌ๐™– ๐™Ÿ๐™–๐™ข๐™ž๐™ž ๐™ฏ๐™ž๐™ก๐™ž๐™ฏ๐™ค ๐™ ๐™–๐™ง๐™ž๐™—๐™ช ๐™ฃ๐™– ๐™ข๐™–๐™š๐™ฃ๐™š๐™ค ๐™ฎ๐™–๐™ก๐™ž๐™ฎ๐™ค๐™๐™ž๐™›๐™–๐™™๐™๐™ž๐™ฌ๐™–.โ€

Grace aliwasilisha matokeo yake kitaifa na kimataifa na ๐ค๐ฎ๐œ๐ก๐š๐ฉ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฃ๐š๐ซ๐ข๐๐š ๐ฅ๐š ๐“๐ซ๐จ๐ฉ๐ข๐œ๐š๐ฅ ๐‚๐จ๐ง๐ฌ๐ž๐ซ๐ฏ๐š๐ญ๐ข๐จ๐ง ๐’๐œ๐ข๐ž๐ง๐œ๐ž. Mwaka 2025 baada ya kumaliza shahada yake ya Uzamili, alijiunga na STEP k**a Afisa wa MEL, ๐ง๐š ๐ฌ๐š๐ฌ๐š ๐ง๐ข ๐Œ๐ซ๐š๐ญ๐ข๐›๐ฎ ๐ฐ๐š ๐Œ๐„๐‹ ๐œ๐ก๐ข๐ง๐ข ๐ฒ๐š ๐Œ๐ค๐š๐ค๐š๐ญ๐ข ๐ฐ๐š ๐Œ๐š๐ง๐๐ก๐š๐ซ๐ข ๐ฒ๐š ๐”๐๐ณ๐ฎ๐ง๐ ๐ฐ๐š.

๐’๐š๐Ÿ๐š๐ซ๐ข ๐ฒ๐š ๐†๐ซ๐š๐œ๐ž ๐ข๐ง๐š๐š๐ค๐ข๐ฌ๐ข ๐๐ก๐š๐ฆ๐ข๐ซ๐š ๐ฒ๐ž๐ญ๐ฎ ๐ฒ๐š ๐ค๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐ž๐ณ๐š ๐ค๐š๐ญ๐ข๐ค๐š ๐ฏ๐ข๐ฉ๐š๐ฃ๐ข ๐ฏ๐ฒ๐š ๐ง๐๐š๐ง๐ข ๐ง๐š ๐ค๐ฎ๐ฃ๐ž๐ง๐ ๐š ๐ฎ๐จ๐ง๐ ๐จ๐ณ๐ข ๐ฐ๐š ๐ฎ๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข ๐ฐ๐š ๐ฆ๐ฎ๐๐š ๐ฆ๐ซ๐ž๐Ÿ๐ฎ. Kwa kuimarisha utafiti, ujifunzaji na ushirikishwaji wa jamii, tunajenga kizazi kijacho cha wanasayansi wa uhifadhi watakaolinda mandhari yetu kwa miaka mingi ijayo.

๐‡๐จ๐ง๐ ๐ž๐ซ๐š ๐ฌ๐š๐ง๐š, ๐†๐ซ๐š๐œ๐ž! ๐Ÿ‘๐ŸŒฟ ๐Š๐ฎ๐ฃ๐ข๐ญ๐ฎ๐ฆ๐š ๐ค๐ฐ๐š๐ค๐จ ๐ง๐š ๐ฎ๐ค๐ฎ๐š๐ฃ๐ข ๐ฐ๐š๐ค๐จ ๐ง๐ข ๐ก๐š๐ฆ๐š๐ฌ๐š ๐ฒ๐š ๐ค๐ฐ๐ž๐ฅ๐ข ๐ค๐ฐ๐š ๐ฃ๐š๐ฆ๐ข๐ข ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ก๐ข๐Ÿ๐š๐๐ก๐ข.

#

Want your organization to be the top-listed Non Profit Organization in Iringa?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Address


P. O. Box 2494
Iringa