Ofisi ya Rais - Tamisemi
Prime Minister’s Office, Regional Administration, and Local Governments (TAMISEMI) is a government Ministry under the Prime Minister’s office.
06/07/2026
Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa anayeshughulikia miundombinu Mhandisi Rogatus Matavilla atembelea banda la Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI lililopo viwanja vya Mwalimu Nyerere Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam leo juni 6,2026
28/06/2026
SIMIYU,MWANZA MABINGWA MPIRA WA WAVU
Na OWM-TAMISEMI,Iringa
Timu ya Mpira wa Wavu Wasichana kutoka Mkoa wa Simiyu, imetetea ubingwa wake baada ya kuibuka na ushindi katika mchezo wa fainali ya UMISSETA iliyochezwa leo tarehe 27 juni 2026.
Mchezo huo wa fainali umechezwa katika viwanja vya Chuo cha ualimu Kleruu Manispaa ya Iringa Mkoani humo, ambapo mashindano ya mwaka huu yanafanyika kitaifa.
Simiyu imeifunga timu ya Mkoa wa Mbeya Seti 3-0, katika mchezo ambao ulikuwa wa kusisimua muda wote.
Kwa upande wa Wavulana mkoa wa Mwanza umetwaa ubingwa kwa kupata ushindi wa seti 3-0 dhidi ya Mbeya.
Mkoa wa Mbeya uliingiza timu mbili katika hatua ya fainali, hali inayoashiria kukua kwa mchezo huo mkoani humo kwa miaka ya hivi karibuni.
Fainali hiyo inahitimisha rasmi michezo ya mpira wa Wavu katika UMISSETA 2026, mashindano ambayo yanatarajiwa kuhitimishwa rasmi tarehe 28 Juni 2026.
27/06/2026
Songwe Yatwaa Ubingwa wa Handball UMISSETA 2026
OWM-TAMISEMI,Iringa
Timu za Mpira wa Mikono (Handball) wavulana na wasichana kutoka Mkoa wa Songwe, zimeibuka kuwa mabingwa katika mashindano ya UMISSETA 2026.
Fainali ya michezo hiyo imechezwa leo tarehe 27 Juni 2026 katika viwanja vya Shule ya Sekondari Iringa Wasichana.
Kwa upande wa wavulana, Mkoa wa Songwe umeshinda magoli 30-29 dhidi ya Morogoro katika mchezo uliokuwa wa kasi na kuvutia kwa dakika zote.
Nayo timu ya wasichana kutoka mkoa wa Songwe, ilifuata nyayo za kaka zao, kufuatia ushindi wa magoli 24-15 ilioupata dhidi ya timj ya Mkoa wa Tabora.
Fainali hiyo imehitimisha rasmi michezo ya Handball katika mshindano ya UMISSETA 2026, ambayo yanafanyika kitaifa mkoani Iringa.
Emmanuel Majura Mratibu wa Handball amesema Mkoa wa Songwe umeweza kupata ushindi huo kutokana na maandalizi mazuri iliyoyafanya.
Pia amezungumzia juu ya ushindani mkubwa ulioshuhudiwa mwaka huu, akieleza kuwa ulitokana na kuongezeka kwa hamasa ya mchezo huo katika mikoa mbalimbali.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the organization
Telephone
Website
Address
Goverment City, Mtumba. TAMISEMI Street
Dodoma