Showbuzz tv
π¬ Showbuzz TV
π₯ Your #1 plug for trending entertainment news
πΆ Music β’ Celebrities β’ Viral Stories
π°πͺ Kenya | East Africa
π© DM for features & promotions WhatsApp +254792246538
Gossips | News | Interviews | Promotions | Digital marketing
14/06/2026
π OMBI LA MHUBIRI EZEKIEL ODERO LATIMIA? WEMA SEPETU APATA MTOTO BAADA YA MIAKA YA KUSUBIRI πΆβ€οΈ
Miaka kadhaa iliyopita, Mhubiri maarufu wa Kenya Ezekiel Odero aligusa mioyo ya wengi baada ya kutoa ombi maalum kwa Mungu kuhusu mwanamke maarufu aliyekuwa amesema hadharani kuwa amekata tamaa ya kupata mtoto kutokana na kusubiri kwa muda mrefu.
Katika maombi yake, Mhubiri Ezekiel alisema:
π£οΈ "Nimemwona mtu maarufu akisema amekata tamaa ya kupata mtoto. Na akasema kwamba labda ni mapenzi ya Mungu. Huenda asinijue, lakini nilimwona kwenye YouTube. Ninaomba Mungu umjibu mwanamke huyo ambaye alisema ana umri wa miaka 30 na hajawahi kupata mtoto."
Leo hii, wengi wanahusisha maneno hayo na Wema Sepetu, ambaye hatimaye amebarikiwa kupata mtoto baada ya safari ndefu iliyokuwa imejaa changamoto, subira na matumaini.
Habari za ujio wa mtoto huyo zimepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki pamoja na wadau wa burudani Afrika Mashariki, huku wengi wakieleza kuwa ni ushuhuda wa kutokata tamaa na kuendelea kuamini.
π Hongera kwa Wema Sepetu na familia yake kwa baraka hii mpya. Hakika furaha huja kwa wakati wake.
π Unalizungumziaje suala hili? Je, unaamini kuwa huu ni ushuhuda wa imani, subira na neema ya Mungu? Tuambie maoni yako.
TrendingNews EastAfricaEntertainment
14/06/2026
πΆ MBOSSO AHOJI UAMUZI WA SUSUMILA KUTOA AUDIO BILA VIDEO KWA MIAKA MITATU π₯
Msanii wa Bongo Fleva Mbosso aliwahi kugusia suala la kuchelewa kutoka kwa video ya wimbo wake na msanii wa Kenya Susumila, akieleza kuwa ni jambo la kushangaza kuona audio ya wimbo ikikaa kwa takribani miaka mitatu bila kupata video rasmi.
Kwa mujibu wa Mbosso, muda huo ni mrefu kwa msanii anayepambana kufikia malengo makubwa ya muziki, kwani video ni sehemu muhimu ya kuongeza thamani na kufikisha kazi kwa mashabiki wengi zaidi.
Wimbo huo wa "Sonona", uliowakutanisha Mbosso na Susumila, uliweza kufanya vizuri na kupata watazamaji wengi licha ya kutokuwa na video rasmi kwa kipindi kirefu. Kauli ya Mbosso ilionekana kuwagusa mashabiki wengi waliokuwa wakisubiri kuona taswira ya wimbo huo.
Je, unaona ni sahihi kwa msanii kusubiri miaka mitatu ndipo atoe video ya wimbo ambao tayari umefanya vizuri? Tuambie maoni yako.
πΊ Showbuzz TV Updates EntertainmentNews EastAfricaMusic
13/06/2026
SHOWBUZZ TV UPDATES πΆπ₯
Msanii Pelzy Never Mind amewafanya mashabiki wake kucheka baada ya kutoa kauli ya utani akimhusisha staa wa Bongo Fleva Jay Melody.
"Siwezi kuskiza ngoma za Jay Melody, hata mimi najua kuimba love song. Kwanza kesho video inashuka kwa mpigo, wacha video ya Jasho itatoka baadaye." π
π€
Kauli hiyo imekuja wakati Pelzy Never Mind akitangaza rasmi kuwa video yake mpya ya mapenzi itaachiwa kesho, huku akiweka pembeni kwa muda video ya "Jasho" ambayo mashabiki wengi walikuwa wakiisubiri.
Je, Pelzy Never Mind anaweza kuleta ushindani mpya kwenye nyimbo za mapenzi na kuwavutia mashabiki k**a anavyodai? π€π₯
π Unasubiri video gani zaidi, ya love song mpya au "Jasho"? Tuambie maoni yako kwenye comment.
Jasho MusicUpdates
Raha tu kwa wema sepetu na whozu
Click here to claim your Sponsored Listing.
Contact the business
Telephone
Address
East Africa
Mombasa